logo blog

Usaili wa mafunzo ngazi ya Tabibu Msaidizi kwenda Afisa Tabibu 2013/14

TANGAZO LA USAILI WA MAFUNZO NGAZI YA TABIBU MSAIDIZI
KWENDA AFISA TABIBU KWA NJIA YA MASAFA MWAKA 2013/14

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inawatangazia wale walioomba kujiunga na mafunzo ya Tabibu Msaidizi kwenda Afisa Tabibu kwa njia ya masafa kuwa kutakua na usaili katika vituo/kanda walizopeleka maombi yao. Usaili huo utafanyika siku ya Jumanne tarehe 25 Machi 2014 kwenye vituo vya mafunzo vya kanda walikotuma maombi yao.


Mwombaji ahakikishe anafika kwenye usaili na vielelezo vifuatavyo:


Awe na cheti halisi cha taaluma (Clinical Assistant)


Awe na cheti halisi cha kuhitimu elimu ya sekondari chenye ufaulu wa walau


daraja la ‘D’ kwa somo la biolojia


Awe amehitimu mafunzo ya Tabibu Msaidizi kuanzia mwaka 2009 hadi 2011.


Kwa maelezo ya ziada kuhusu zoezi hili la usaili fika kwenye ofisi ya Kanda uliyotuma maombi yako.


Orodha ya majina ya waombaji walioitwa kwenye usaili katika kila kanda ni haya

yafuatayo:- Bofya hapa kupakua faili lenye orodha ya majina